|
Dira ya HakiElimu ni kuona kuwa kila mtoto
wa Tanzania anapata haki yake ya kupatiwa elimu bora ya msingi
katika shule zinazojali na kuheshimu utu, kukuza ubunifu na
kuwawezesha wanafunzi kujifunza bila woga kwa kuuliza maswali,
kutoa changamoto na kutafakari kwa kina na kuinua haki za
binadamu na demokrasia.
Sisi HakiElimu tunaamini kuwa elimu nchini
Tanzania itaimarika na kuboreshwa zaidi iwapo sote tutashiriki
kikamilifu. Kwa sababu hiyo hatujaribu kutatua matatizo mengi
sisi wenyewe, bali tunatafuta na kutoa nafasi na fursa kwa
wananchi wenyewe kutatua matatizo hayo wao wenyewe!

Tovuti hii itakupatia taarifa zaidi kuhusu
Dira ,Dhamira
malengo, mikakati na programu
zetu pamoja na historia yetu. Inajumuisha pia uchambuzi wetu
wa hali ya elimu nchini Tanzania na kukuunganisha na nyaraka
nyingine muhimu. (Bonyeza hapa
ili kuweza kupata kipeperushi kinachoelezea kwa ufupi shughuli
zetu kikiwa katika mfumo wa zip file). Tovuti hii itakupa
mwanga kuhusu HakiElimu na muktadha/mazingira ya kazi yetu,
hata hivyo iwapo utakuwa na maswali zaidi, tafadhali usisite
kuwasiliana nasi.
Aidha, tungependa kufahamu kuhusu wewe,
mawazo na dukuduku zako kuhusu elimu nchini Tanzania! Tafadhali
piga kura yako ya maoni au
toa maoni yako katika sehemu maalumu
hapo pembeni au wasiliana nasi.
Tutachangia maoni yako na watu wengine ikiwa ni pamoja na
wale wanaofanya maamuzi. Tuandikie na utusaidie kuleta mabadiliko
katika elimu nchini Tanzania.
|